Na Mwandishi Wetu-Kigoma
Wakazi wa kijiji cha Mkwanga halmashauri ya wilaya ya Kigoma, wanakabiliwa na hatari za kiafya kutokana na kulazimika kutumia maji machafu yanayopita katika mtaro unaopeleka maji katika mto Kaseke wilayani humo,na hivyo wameiomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto hiyo.
Wakielezea kuhusiana na maji wanayotumia, wakazi wa kijiji hicho wamesema licha ya kuona takataka kwenye maji hayo lakini bado wamekuwa wakilazimika kuyatumia tu kutokana na kutokuwa na mbadala.

Amina Bahita ni mkazi wa kijiji cha Mkwanga ameeleza kuwa hali hiyo imekuwa ikiwaathiri kiafya ikiwemo kuwa sababishia kuugua matumbo na kichocho
“Haya maji hayana usalama kabisa yana safirisha takataka kutoka maeneo mengine halafu tunachangia na mifugo kama ng’ombe na mbwa hii sio sawa “Amesema Bahita
Naye mwenyekiti wa kijiji cha Mkwanga Paulo Ntibalio ameeleza kero hiyo inapaswa kupatiwa ufumbuzi wa haraka hatua itakayo saidia usalama wa wananchi katika eneo hilo na kuepukana na madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi ya maji yasiyo salama.

Alieleza wamekuwa wakijitahidi kuzuia shughuli za kibinadamu zinazo chafua mto huo ikiwemo viwanda vya Mawese vinavyo mwaga taka katika mto huo lakini wameshindwa kudhibiti uchafuzi huo.
Kituo hiki kimemtafuta meneja wa RUWASA wilaya ya Kigoma Respicious Mombeki kufahamu juu ya suala hilo ambapo ameeleza eneo hilo lilipaswa wananchi waanze kutumia maji safi na salama tangu mwezi wa tano mwaka jana
Alieleza kinacho kwamisha hadi sasa ni mkandarasi anae tekeleza mradi huo Serengeti limited Company kushindwa kukamilisha kwa wakati huku akiwa ameshaongezewa muda kwa awamu tatu bila mafanikio.
“Inawezekana mkandarasi hana uwezo au ana miradi mingi sisi kama RUWASA tunapambana kuhakikisha ananyang’anywa huo mradi ili tuumalizie na wananchi wapate maji” Amesema Mombeki
Alieleza kinacho sababisha washindwe kuchukua hatua za haraka dhidi ya mkandarasi huyo ni kuwa aliingia mkataba na mfadhili wa mradi huo shirika la ENABEL na sio wao .
Habari Zaidi
DCI KINGAI ASISITIZA WAZAZI KUZINGATIA MALEZI BORA KWA WATOTO WAO ILI KUPUNGUZA UKATILI
THRDC,C-SEMA YAENDESHA MAFUNZO KWA POLISI NA WAENDESHA MASHITAKA