Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliyeanza ziara yake ya kihistoria nchini Rwanda ameiomba radhi nchi hiyo kufuatia mauji ya kimbari ya mwaka 1994 kwa kuwa Ufaransa ilikuwa na wajibu mkubwa na wa kihistoria kuwajibikaji dhidi ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda.
“Nimesimama hapa mbele yenu leo kwa unyenyekevu na heshima kubwa,nimetambua uwajibikaji wa Ufaransa ulikuwa muhimu” amesema Rais Macron mwanzoni mwa hotuba yake aliyoitoa eneo la makumbusho ya mauaji ya Kimbari,yalipohifadhiwa mabaki ya watu 250,000 waliouawa katika mapigano ya kikabila miaka 27 iliyopita.
Macron amekuwa rais wa kwanza wa Ufaransa kuitembelea Rwanda baada ya miaka kumi ya kigugumizi kwa Ufaransa dhidi ya mauji ya maelfu ya Wanyarwanda,wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi.
Rais Macron amewasili kwa ziara ya kihistoria, kurejesha uhusiano baina ya nchi hizo mbili zilizokuwa na uhusiano wa kihistoria uliokuwa umepotea kwa mwaka 27,na amekaribishwa vyema na mwenyeji wake Paul Kagame ambae amempongeza kwa kutambua umuhimu wa Ufaransa na uwajibikaji kufuatia mauaji ya Kimbari.
“Maneno yake yamekuwa ya thamani kuliko hata msamaha wenyewe,na ni yakweli”,amesema Rais Kagame alipozungumza na wanahabari mara baada ya mazungumzo yake na Rais Macron mjini Kigali.
Kiongozi mkuu wa chama cha manusura wa mauaji ya kimbari (IBUKA) Egide Nkuranga amesema hotuba ya Macron haikuwa na matumaini makubwa na ni ya kukatisha tamaa maana hajaomba msamaha wa kueleweka kwa niaba ya Ufaransa wala hajaomba kusamehewa.
“Amejaribu tu kuelezea mauaji na wajibu wa Ufaransa,na hii ni sawa maana anaonesha dhahiri kuwa anajua ukweli”,amesema Nkuranga alipokosoa hotuba ya Macron.
Ufaransa ilihusikaje na mauaji ya kimbari?
Matokeo ya ripoti mbili zilizotolewa mwezi March na April mwaka huu kuhusu jukumu la Ufaransa kwa Rwanda zilibainisha uwezekano wa Ufaransa kuhusika katika mauaji yale.Ripoti hizo mbili zilizokabidiwa kwa rais Macron ziliishtumu Ufaransa kuhusika katika umwagaji damu nchini Rwanda kwa namna moja ama nyingine.
Matokeo ya ripoti hizo,yaliyokubaliwa na Serikali ya Ufaransa, yanaituhumu Ufaransa kuhusika katika mauaji hayo kwa kuwa ilikuwa karibu zaidi utawala uliokuwa madarakani wa kabila la Wahutu.Hata hivyo hapakuwa na ushahidi wa moja kwa moja juu Ufaransa kuhusika katika umwagaji damu japo wengi wa waliouawa walikuwa ni kabila hasimu la Watutsi.
Habari Zaidi
ETHIOPIA: AJIUNGA CHUO KIKUU AKIWA NA MIAKA 69
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO
KENYA: ODINGA AMTEUA MARTHA KARUA KUWA MGOMBEA MWENZA WA URAIS