March 23, 2023

Watetezi Media

Official Website for Watetezi Media

TANZANIA,RWANDA ZAAHIDI KUKUZA USHIRIKIANO

Rais Samia Suluhu akiwa na mjumbe maalum kutoka Rwanda

Rais Samia suluhu hii leo ameupokea ujumbe maalum  kutoka kwa rais wa Rwanda,Paul kagame uliowasilishwa na Mjumbe maalum na  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Rwanda, Dkt. Vincent Biruta.

Marais wa Tanzania na Rwanda wameahidi kukuza uhusiano na ushirikiano baina ya mataifa hayo mawili hususan katika utekelezaji wa miradi ukiwemo mradi wa kuzalisha umeme wa Rusumo na ujenzi wa reli ya kisasa ya kuunganisha Jiji la Kigali na Isaka (Tanzania) ambayo itasaidia katika usafirishaji wa mizigo kutoka Bandari ya Dar es salaam kwenda Rwanda.

Rais  Kagame kupitia  ujumbe huo maalum ametuma  salamu za pole kufuatia kifo cha aliyekuwa rais wa Tanzania,Hayati Dkt John Pombe Magufuli na kumpongeza Rais Samia Suluhu kwa kupokea kijiti cha urais