Somalia imetangaza kuwa uchaguzi nchini humo utafanyika ndani ya siku 60 zijazo, uamuzi ambao umetolewa baada ya kufanyika kwa mazungumzo ya kisiasa yaliyokuwa yakifanyika katika mji wa Mogadishu nchini humo.
Waziri wa Habari, Abdirahman Yusuf amesema wamekubaliana kuwa uchaguzi ufanyike ndani ya miezi miwili na tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi itatangazwa na Tume ya uchaguzi hapo badae .Naye Waziri Mkuu wa Somalia,Mohamed Hussein Roble amesema hatua iliyofikiwa ni ya kihistoria.
Uchaguzi nchini Somalia ulitarajiwa kufanyika mwezi Februari mwaka huu ukaingiwa na dosari baada ya serikali inayoongozwa na rais Mohamed Abdullahi Farmajo kushindwa kuelewana na viongozi wa majimbo matano juu ya namna ya kuufanikisha uchaguzi huo na Bunge kupitisha mswada wa kumuongezea Rais Farmajo muda wa miaka miwili suala ambalo lilipingwa na upinzani.
Habari Zaidi
BULAYA AHOFIA MUSTAKABALI WA WANAHABARI SAMIA AKIONDOKA MADARAKANI
ETHIOPIA: AJIUNGA CHUO KIKUU AKIWA NA MIAKA 69
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO