Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye na mkewe,Angelina Ndayubaha hii leo anaanza ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Kenya na ziara hiyo itaanzia mjini Kisumu.
Taarifailiyotolewa na ya Ikulu ya Kenya, Rais Ndayishimiye atashiriki katika zoezi la uzinduzi wa miradi mbalimbali ya serikali katika kaunti ya Kisumu na atakuwa mgeni wa heshima wakati rais Uhuru Kenyatta atakapoongoza taifa hilo katika kuadhimisha sherehe za 58 za Siku ya Madaraka zitakazofanyika katika uwanja mpya wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Habari Zaidi
ETHIOPIA: AJIUNGA CHUO KIKUU AKIWA NA MIAKA 69
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO
KENYA: ODINGA AMTEUA MARTHA KARUA KUWA MGOMBEA MWENZA WA URAIS