Watoto wawili Daniel Joseph (14) na Charles Njola (16) wakazi wa kijiji cha Mugera kata ya Nyantakara wilayani Biharamulo mkoani Kagera.
wamethibitishwa kupoteza maisha baada ya kulipukiwa na kitu kinachodaiwa kuwa bomu.
Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi, amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 27 mwaka huu kati ya saa 12 na saa 1:00 jioni, wakati watoto hao wakirejea nyumbani kutoka malishoni walikokwenda kuchunga ng’ombe.
Amesema kuwa watoto hao waliokota chuma ambacho kinadhaniwa kuwa ni bomu na bila kujua walianza kukichezea kabla hakijalipuka.
Kutazama video ya tukio hili bofya link hii:https://youtu.be/1skBMNgQ5_M
Habari Zaidi
DCI KINGAI ASISITIZA WAZAZI KUZINGATIA MALEZI BORA KWA WATOTO WAO ILI KUPUNGUZA UKATILI
THRDC,C-SEMA YAENDESHA MAFUNZO KWA POLISI NA WAENDESHA MASHITAKA