Na Antony Rwekaza
Kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi namba 16/2021 inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake imeibuka kufuatia Mahakamani kupokea mapingamizi mawili yaliyowekwa na mawakili wa upande wa utetezi, wakidai maelezo yanayodiwa kuwa ya mshtakiwa namba tatu Mohamed Ling’wenya yalichukuliwa baada ya mshitakiwa kulazimishwa.
Mawakili wa Jamhuri wameomba kupewa muda wa kujiandaa kwa ajili ya kuaza kusikiliza kesi hiyo ndogo, upande wa utetezi umekubali na Jaji ameiahirisha kesi hiyo mpaka kesho Novemba 10, 2021 saa 5:00 asubuhi.
Ikumbukwe leo shahidi wa nane upande wa Jamhuri alikuwa akiendelea na ushahidi wake hivyo ataendelea anatarajiwa kuendelea na kukamilisha ushahidi baada ya kesi ndogo kukamilika ambayo nayo itajumuisha mashahidi kutoka pande zote, lakini upande wa Jamhuri ndiyo unaotarajiwa kuanza.
Habari Zaidi
KIKOSI KAZI KITASAIDIA KULETA MARIDHIANO – JK
NI MIAKA MITANO SASA TOKEA LISSU ASHAMBULIWE
SHAHIDI JAMHURI AELEZA KINA MBOWE WALIVYOSUKA MPANGO WA KUTENDA UGAIDI