Na Rodrick Mushi, Kilimanjaro
Fisi ameibua taharuki kwa wakazi wa Kijiji cha Kwa Sadala Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro baada ya kuvamia makazi ya watu katika Kitongoji cha Dipu na kuua kondoo saba.
Adam Alex mkazi wa Sadala na ambae pia mifugo yake iliuliwa na fisi huyo ameeleza kuwa fisi huyo aliingia kwenye makazi yao May 20 majira ya usiku na kuingia kwenye nyumba kadhaa za wakazi wa eneo hilo na kuua mifugo.

Diwani wa Kata ya Masama Kusini Cedrick Pangani amekwishafika katika eneo la tukio na kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiwapa pole wanachi waliopoteza mifugo yao na kueleza kuwa tayari mamlaka ya maliasili na utalii imekwishafika Kijijini hapo na kuanza kufanya juhudi za kumsaka fisi huyo ili kuepusha madhara zaidi.

Habari Zaidi
DCI KINGAI ASISITIZA WAZAZI KUZINGATIA MALEZI BORA KWA WATOTO WAO ILI KUPUNGUZA UKATILI
THRDC,C-SEMA YAENDESHA MAFUNZO KWA POLISI NA WAENDESHA MASHITAKA