Raia mmoja wa Ethiopia,Tadesse Ghichile (69) amejiunga na Chuo Kikuu cha Jimma ambako anatarajiwa kuhitimu shahada ya Matibabu.
Ghichile ni baba wa watoto 11,ni mkulima na pia anauza mgahawa kijijini kwake ili aweze kuitunza familia yake.Akiwa yatima katika umri mdogo aliacha shule akiwa darasa la nane.
Takribani miaka 10 iliyopita Ghichile alichukua uamuzi wa kurudi katika mfumo rasmi wa elimu na kufaulu mtihani wa kitaifa wa kuingia chuo kikuu.
Anasema Kwa muda mrefu alikuwa amepata ugumu kurudi shuleni baada ya kuanzisha familia. Lakini alidhamiria kumaliza hadi mwisho.
Habari Zaidi
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO
KENYA: ODINGA AMTEUA MARTHA KARUA KUWA MGOMBEA MWENZA WA URAIS
INDIA : WANNE MBARONI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA KENGE