Kiongozi wa upinzani wa Belarus, Svetlana Tsikhanovskaya amesema kuwa mwanablogu anayeshikiliwa nchini humo, Roman Protasevich amepigwa na kuteswa akiwa jela.
Wakili aliyemtembelea mwandishi huyo na mpenzi wake, Sofia Sapega alisema yuko salama ila Tsikhanovskaya amewaambia waandishi wa habari kuwa taarifa hiyo ni ya kutiliwa mashaka na ukweli ni kuwa aliteswa na kupigwa.
Kiongozi huyo wa upinzani bado hajatoa ushahidi thabiti kuhusiana na madai yake ingawa familia ya mwandishi huyo katika mkanda wa video imesema mkanda huo ulionyesha dalili za mateso nayaopitia mwanablogu huyo kutoka jela
Protasevich na mpenzi wake walikamatwa mnamo Mei 23 mwaka huu baada ya ndege yao kulazimishwa kutua mjini Minsk.
Habari Zaidi
ETHIOPIA: AJIUNGA CHUO KIKUU AKIWA NA MIAKA 69
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO
KENYA: ODINGA AMTEUA MARTHA KARUA KUWA MGOMBEA MWENZA WA URAIS