Mwanamume mmoja nchini Mali anayetuhumiwa kwa kujaribu kumchoma kisu rais wa mpito wa Taifa hilo ,Assimi Goïta juma lililopita amekufa hospitalini akiwa chini ya ulinzi,sababu ya kifo chake inachunguzwa.
Mwanamume huyo, ambaye hajatambuliwa, alikamatwa baada ya kushindwa kutekeleza jaribio hilo la mauaji wakati Goïta alipohudhuria swala msikitini.
Taarifa ya serikali imesema afya ya mtu huyo ilikuwa imezorota akiwa chini ya ulinzi na alipelekwa hospitalini.
Habari Zaidi
ETHIOPIA: AJIUNGA CHUO KIKUU AKIWA NA MIAKA 69
MWANDAAJI MISS RWANDA KUFUNGULIWA MASHITAKA YA UHALIFU WA KINGONO
KENYA: ODINGA AMTEUA MARTHA KARUA KUWA MGOMBEA MWENZA WA URAIS